Hassan Mambosasa ni mzaliwa wa mkoa wa Tanga nchini Tanzania, elimu yake ameipata kwenye shule mbalimbali za sekondari. Ikiwemo Jitegemee JKT, Wailes, Ubungo islamic, victory na kuja kuhitimu kidato cha sita kwenye shule ya sekondari Tambaza. Elimu ya juu aliipata chuo kikuu cha kilimo cha Sokoine (SUA), amesomea masuala ya TEHAMA akishughulika zaidi kwenye vifaa vya kompyuta. Alianza uandishi mnamo mwaka 2006 hadi hii leo ameandika hadithi zaidi ya 40 katika mfumo wa vitabu vya mtandaoni.
Bazazi.
Par :Formats :
Disponible dans votre compte client Decitre ou Furet du Nord dès validation de votre commande. Le format ePub est :
- Compatible avec une lecture sur My Vivlio (smartphone, tablette, ordinateur)
- Compatible avec une lecture sur liseuses Vivlio
- Pour les liseuses autres que Vivlio, vous devez utiliser le logiciel Adobe Digital Edition. Non compatible avec la lecture sur les liseuses Kindle, Remarkable et Sony
, qui est-ce ?Notre partenaire de plateforme de lecture numérique où vous retrouverez l'ensemble de vos ebooks gratuitement
Pour en savoir plus sur nos ebooks, consultez notre aide en ligne ici
- FormatePub
- ISBN8233223747
- EAN9798233223747
- Date de parution24/01/2026
- Protection num.pas de protection
- Infos supplémentairesepub
- ÉditeurLinda Balsamo
Résumé
Ndoa ya kijana msomi wa chuo kikuu inaingiliwa na jinamizi, mke ambaye naye ni msomi aliamua kuangukia mikononi mwa kijana wa Waziri. Licha ya kumuoa kwa ndoa halali, bado aliporwa na mwanamke kuishi kwa mwanaume mwingine. Familia ya kijana ni masikini ilishindwa kumsaidia kwenye janga hilo, familia ya binti inaishia kumgeuka na kuungana na bwana mpya baada ya kuhongwa pesa nyingi. Kijana alibaki hana msaada, haikuchukua muda mrefu alipata ajali isiyoeleweka na kutangazwa kafariki. Ndugu walipotaka kufanyiwa uchunguzi mwili wake, polisi nao waliamua kuingilia matokeo walizuiwa kuuosha mwili.
Walipewa ukiwa umeoshwa na kuvishwa sanda, waliamriwa kuuzika pasipo kufanya ibada ya kumuaga kwa mujibu wa dini yake. Jambo hilo lilifanyika na ikapita juma moja, ndiyo hapo barua ikaja kufika mezani kwa Norbert Kaila. Mwananchi akisimulia kuhusiana na hilo, akiomba msaada kutoka kwake kama mwandishi wa habari.. Norbert Kaila aliingia kazini, na hapo ndiyo yalibainika mazito kuhusiana na kifo cha kijana yule.
Ambacho hakikutokana na wivu wa mapenzi kama wengi walivyohisi.
Walipewa ukiwa umeoshwa na kuvishwa sanda, waliamriwa kuuzika pasipo kufanya ibada ya kumuaga kwa mujibu wa dini yake. Jambo hilo lilifanyika na ikapita juma moja, ndiyo hapo barua ikaja kufika mezani kwa Norbert Kaila. Mwananchi akisimulia kuhusiana na hilo, akiomba msaada kutoka kwake kama mwandishi wa habari.. Norbert Kaila aliingia kazini, na hapo ndiyo yalibainika mazito kuhusiana na kifo cha kijana yule.
Ambacho hakikutokana na wivu wa mapenzi kama wengi walivyohisi.






















