Ndoa ya kijana msomi wa chuo kikuu inaingiliwa na jinamizi, mke ambaye naye ni msomi aliamua kuangukia mikononi mwa kijana wa Waziri. Licha ya kumuoa kwa ndoa halali, bado aliporwa na mwanamke kuishi kwa mwanaume mwingine. Familia ya kijana ni masikini ilishindwa kumsaidia kwenye janga hilo, familia ya binti inaishia kumgeuka na kuungana na bwana mpya baada ya kuhongwa pesa nyingi. Kijana alibaki hana msaada, haikuchukua muda mrefu alipata ajali isiyoeleweka na kutangazwa kafariki. Ndugu walipotaka kufanyiwa uchunguzi mwili wake, polisi nao waliamua kuingilia matokeo walizuiwa kuuosha mwili.
Walipewa ukiwa umeoshwa na kuvishwa sanda, waliamriwa kuuzika pasipo kufanya ibada ya kumuaga kwa mujibu wa dini yake. Jambo hilo lilifanyika na ikapita juma moja, ndiyo hapo barua ikaja kufika mezani kwa Norbert Kaila. Mwananchi akisimulia kuhusiana na hilo, akiomba msaada kutoka kwake kama mwandishi wa habari.. Norbert Kaila aliingia kazini, na hapo ndiyo yalibainika mazito kuhusiana na kifo cha kijana yule.
Ambacho hakikutokana na wivu wa mapenzi kama wengi walivyohisi.
Ndoa ya kijana msomi wa chuo kikuu inaingiliwa na jinamizi, mke ambaye naye ni msomi aliamua kuangukia mikononi mwa kijana wa Waziri. Licha ya kumuoa kwa ndoa halali, bado aliporwa na mwanamke kuishi kwa mwanaume mwingine. Familia ya kijana ni masikini ilishindwa kumsaidia kwenye janga hilo, familia ya binti inaishia kumgeuka na kuungana na bwana mpya baada ya kuhongwa pesa nyingi. Kijana alibaki hana msaada, haikuchukua muda mrefu alipata ajali isiyoeleweka na kutangazwa kafariki. Ndugu walipotaka kufanyiwa uchunguzi mwili wake, polisi nao waliamua kuingilia matokeo walizuiwa kuuosha mwili.
Walipewa ukiwa umeoshwa na kuvishwa sanda, waliamriwa kuuzika pasipo kufanya ibada ya kumuaga kwa mujibu wa dini yake. Jambo hilo lilifanyika na ikapita juma moja, ndiyo hapo barua ikaja kufika mezani kwa Norbert Kaila. Mwananchi akisimulia kuhusiana na hilo, akiomba msaada kutoka kwake kama mwandishi wa habari.. Norbert Kaila aliingia kazini, na hapo ndiyo yalibainika mazito kuhusiana na kifo cha kijana yule.
Ambacho hakikutokana na wivu wa mapenzi kama wengi walivyohisi.